Chapter 23 of 150

Zaburi23

Bwana ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu.

Hunilaza katika malisho ya majani mabichi, kando ya maji matulivu huniongoza,

hunihuisha nafsi yangu. Huniongoza katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.

Hata kama nikipita katikati ya bonde la uvuli wa mauti, sitaogopa mabaya, kwa maana wewe upo pamoja nami; fimbo yako na mkongojo wako vyanifariji.

Waandaa meza mbele yangu machoni pa adui zangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, kikombe changu kinafurika.

Hakika wema na upendo vitanifuata siku zote za maisha yangu, nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele.

Zaburi 23 · KJV Audio
0:00
0:00