Chapter 129 of 150

Zaburi129

Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:

wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.

Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.

Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.

Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.

Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua;

kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake.

Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya Bwana iwe juu yako; tunakubariki katika jina la Bwana.”

Zaburi 129 · KJV Audio
0:00
0:00